“Kuwa tajiri si kazi rahisi. Ukipata milioni ya kwanza utataka nyingine kulinda hiyo ya kwanza. Ukipata ya pili utataka mbili zingine kulinda hizo mbili za kwanza, n.k. Si kazi rahisi. Si kama unavyofikiria. Utajiri haujanipa furaha. Umenipa uhuru. Ndugu zangu ni maskini wa kutupwa. Ningependa kuishi kama maskini mwenye pesa nyingi.”

Enock Maregesi

Enock Maregesi - “Kuwa tajiri si kazi rahisi. Ukipata...” 1

Similar quotes

“Heri kuwa maskini mwenye pesa nyingi kuliko tajiri mwenye mifuko iliyotoboka.”

Enock Maregesi
Read more

“Usalama wa Taifa ni akili si ukali. Kazi yake, au wajibu wake; ni kukusanya, kuchanganua, kudurusu na kuunganisha kwa makini, taarifa nyeti za kijasusi za ndani na nje ya nchi kuilinda Tanzania na watu wake. Ukitaka kuwa na akili kuwa kawaida. Ukitaka kuwa na nguvu kuwa mkarimu. Ukitaka kuwa tajiri kuwa tajiri wa unyenyekevu.”

Enock Maregesi
Read more

“Zawadi bora ya maisha kwa mwanadamu si fursa ya kufanya kazi kwa bidii na kuwa kitu fulani katika jamii. Ni amani ya Mungu katika moyo wa mwanadamu.”

Enock Maregesi
Read more

“Iwapo kila mtu atamheshimu mwenzake kama anavyojiheshimu mwenyewe; tunaweza kuishi mbinguni duniani ... lakini kwanza tuwe na maarifa binafsi.”

Enock Maregesi
Read more

“Kitu cha kwanza kufanya kama umeamua kuficha ukweli wape watu ukweli mwingine.”

Enock Maregesi
Read more