“Serikali haifungi mtu kutokana na shinikizo la watu. Inafunga mtu kutokana na sheria za nchi.”

Enock Maregesi

Explore This Quote Further

Quote by Enock Maregesi: “Serikali haifungi mtu kutokana na shinikizo la w… - Image 1

Similar quotes

“Watu wanaohatarisha maisha yao kwa kudharau sheria wakati mwingine hawatakiwi kudharauliwa. Ni sawa na mtu aliyepoteza kila kitu katika maisha yake. Wana uwezo wa kufanya chochote.”


“Usalama wa Taifa ni akili si ukali. Kazi yake, au wajibu wake; ni kukusanya, kuchanganua, kudurusu na kuunganisha kwa makini, taarifa nyeti za kijasusi za ndani na nje ya nchi kuilinda Tanzania na watu wake. Ukitaka kuwa na akili kuwa kawaida. Ukitaka kuwa na nguvu kuwa mkarimu. Ukitaka kuwa tajiri kuwa tajiri wa unyenyekevu.”


“Iwapo kila mtu atamheshimu mwenzake kama anavyojiheshimu mwenyewe; tunaweza kuishi mbinguni duniani ... lakini kwanza tuwe na maarifa binafsi.”


“Ukiishi Mexico City katika daraja la watu wakubwa na wewe na anasa ni marafiki wakubwa, hutapenda kuendesha gari ambayo kila mtu anaendesha mjini. Nunua gari na kuibadilisha kuwa ya kwako. Lisa aliponunua gari yake huko Ejército Nacional Mexicano, Mexico City, katika duka la Ferrari, aliipeleka Los Angeles kwa marekebisho aliyoyataka. Ferrari haikuwa ya kawaida. Mbali na kinga ya risasi ya inchi nne, Ferrari ya Lisa ilikuwa na mwendo mkali na matairi makubwa kuliko Ferrari za kawaida. Ilikuwa na rangi tatu: nyeusi, pinki na njano zilizokuwa zikibadilika kulingana na hali ya hewa; na kadhalika ilikuwa na breki ya upepo kwa nyuma, katika buti ya aluminiamu, kwa ajili ya kuikandamiza chini wakati wa mwendo mkali, ili isiyumbe sana barabarani. Lisa peke yake ndiye aliyekuwa na gari ya namna hiyo Mexico City nzima.”


“Nimebadili utaratibu wangu siku hizi kutokana na maadili ya watoto wetu. Siongei na watoto wangu kuhusu Mungu. Naongea na Mungu kuhusu watoto wangu. Yesu alilipa gharama ya maisha yake kutununua kutoka kwa Shetani. Tumrudie; hususan katika kipindi hiki ambacho dunia imekata tamaa.”


“Kila mtu hapa duniani ni jirani yako. Hakuna mtu mwingine hapa ulimwenguni isipokuwa sisi. Lazima tujifunze kuishi pamoja.”