“Usalama wa Taifa ni akili si ukali. Kazi yake, au wajibu wake; ni kukusanya, kuchanganua, kudurusu na kuunganisha kwa makini, taarifa nyeti za kijasusi za ndani na nje ya nchi kuilinda Tanzania na watu wake. Ukitaka kuwa na akili kuwa kawaida. Ukitaka kuwa na nguvu kuwa mkarimu. Ukitaka kuwa tajiri kuwa tajiri wa unyenyekevu.”

Enock Maregesi

Enock Maregesi - “Usalama wa Taifa ni akili si ukali...” 1

Similar quotes

“Zawadi bora ya maisha kwa mwanadamu si fursa ya kufanya kazi kwa bidii na kuwa kitu fulani katika jamii. Ni amani ya Mungu katika moyo wa mwanadamu.”

Enock Maregesi
Read more

“Mojawapo ya misingi ya ujasusi ni kuwa na uwezo wa kutofautisha kati ya unachojua, usichojua na unachofikiria. Unaweza kusema unajua wakati hujui. Maamuzi yasiyo sahihi ya kijasusi huweza kuiletea tume madhara makubwa.”

Enock Maregesi
Read more

“Kufanikiwa katika maisha ni kuwa tayari muda wowote kujitoa mhanga kwa ajili ya kitu unachoweza kuwa.”

Enock Maregesi
Read more

“Ukiishi Mexico City katika daraja la watu wakubwa na wewe na anasa ni marafiki wakubwa, hutapenda kuendesha gari ambayo kila mtu anaendesha mjini. Nunua gari na kuibadilisha kuwa ya kwako. Lisa aliponunua gari yake huko Ejército Nacional Mexicano, Mexico City, katika duka la Ferrari, aliipeleka Los Angeles kwa marekebisho aliyoyataka. Ferrari haikuwa ya kawaida. Mbali na kinga ya risasi ya inchi nne, Ferrari ya Lisa ilikuwa na mwendo mkali na matairi makubwa kuliko Ferrari za kawaida. Ilikuwa na rangi tatu: nyeusi, pinki na njano zilizokuwa zikibadilika kulingana na hali ya hewa; na kadhalika ilikuwa na breki ya upepo kwa nyuma, katika buti ya aluminiamu, kwa ajili ya kuikandamiza chini wakati wa mwendo mkali, ili isiyumbe sana barabarani. Lisa peke yake ndiye aliyekuwa na gari ya namna hiyo Mexico City nzima.”

Enock Maregesi
Read more

“Kuwa tajiri si kazi rahisi. Ukipata milioni ya kwanza utataka nyingine kulinda hiyo ya kwanza. Ukipata ya pili utataka mbili zingine kulinda hizo mbili za kwanza, n.k. Si kazi rahisi. Si kama unavyofikiria. Utajiri haujanipa furaha. Umenipa uhuru. Ndugu zangu ni maskini wa kutupwa. Ningependa kuishi kama maskini mwenye pesa nyingi.”

Enock Maregesi
Read more