Enock Maregesi was born in Tanzania. He is the author of KOLONIA SANTITA, a novel. In 2015 he won the Mabati-Cornell Kiswahili Prize For African Literature for KOLONIA SANTITA. The prize has the express goal in recognizing excellent writing in African languages and encourages translation from, between and into African languages! He lives in Tanzania.
Enock Maregesi alizaliwa nchini Tanzania. Amesomea teknolojia ya habari na utawala wa biashara katika Chuo Kikuu cha Wales, na uandishi wa habari na vitabu katika chuo cha ubunifu wa kifasihi cha Manchester (The Writers Bureau) nchini Uingereza. Hadithi ya KOLONIA SANTITA: LAANA YA PANTHERA TIGRISI ni kitabu chake cha kwanza kilichohamasishwa na wakongwe wa riwaya wa Tanzania - kama Elvis Musiba, Euphrase Kezilahabi na Ben Mtobwa - na utafiti yakinifu wa miaka kumi na nane wa ujasusi, madawa ya kulevya, ugaidi wa kimataifa na silaha za maangamizi za kikemia na kibiolojia. Alizaliwa huko Mwanza mwaka 1972 na kukulia Musoma na Dar es Salaam ambako anaishi mpaka leo, akijishughulisha na biashara na uandishi wa vitabu.
“Kujamiiana si anasa tena katika maisha yangu. Ni hitaji muhimu kwa ujenzi wa familia.”
“Mapenzi ni kiburudisho kikubwa kuliko vyote katika maisha.”
“Zawadi bora ya maisha kwa mwanadamu si fursa ya kufanya kazi kwa bidii na kuwa kitu fulani katika jamii. Ni amani ya Mungu katika moyo wa mwanadamu.”
“Heri kuogopwa kuliko kupendwa kama huwezi kuogopwa na kupendwa kwa wakati mmoja.”
“Mungu hababaishwi na matatizo yako. Anababaishwa na imani yako.”
“Hekima ni ufunguo wa kufanya maamuzi mema kulingana na msingi wa maarifa ya Biblia.”
“Kucheza muziki si lazima utingishe mwili kama mwendawazimu. Unaweza kucheza kwa hisia.”
“Heri kufuta mashtaka kuliko kumfunga mtuhumiwa asiyekuwa na makosa. Kuonewa kunauma.”
“Serikali haifungi mtu kutokana na shinikizo la watu. Inafunga mtu kutokana na sheria za nchi.”
“Uraibu ni mbaya unapoathiri maisha ya mtu.”
“Usitegemee malaika ashuke kutoka mbinguni kuja kukutatulia shida zilizokushinda kwa uzembe. Malaika ni wewe mwenyewe. Ukifanya unachoweza kufanya, Mungu atafanya usichoweza kufanya.”
“Mojawapo ya misingi ya ujasusi ni kuwa na uwezo wa kutofautisha kati ya unachojua, usichojua na unachofikiria. Unaweza kusema unajua wakati hujui. Maamuzi yasiyo sahihi ya kijasusi huweza kuiletea tume madhara makubwa.”
“Heri kuwa maskini mwenye pesa nyingi kuliko tajiri mwenye mifuko iliyotoboka.”
“Kuwa tajiri si kazi rahisi. Ukipata milioni ya kwanza utataka nyingine kulinda hiyo ya kwanza. Ukipata ya pili utataka mbili zingine kulinda hizo mbili za kwanza, n.k. Si kazi rahisi. Si kama unavyofikiria. Utajiri haujanipa furaha. Umenipa uhuru. Ndugu zangu ni maskini wa kutupwa. Ningependa kuishi kama maskini mwenye pesa nyingi.”
“Watu wa kulisaidia bara la Afrika hawatatoka Amerika au kwingineko. Afrika ni tatizo letu. Watatoka Afrika kwenyewe.”
“Kujiingiza katika madawa ni matokeo ya maisha. Hatutumii madawa ya kulevya. Madawa ya kulevya ni sisi wenyewe; tunahitaji kusaidiwa.”
“Situmii madawa ya kulevya. Madawa ya kulevya ni mimi mwenyewe; nahitaji kusaidiwa!”
“Las Vegas. Madhali umeona tunafanya nini katika maisha, fumba macho kwa kuyakodoa. Wanaosema hawajui wanaojua hawasemi. Siri ni siri milele. Kinachofanyika hapa hubakia hapa.”
“Two plus two is not sometimes equal to four ... It is equal to four plus one because one is a powerful amalgamation.”
“It is quite disappointing that people you love the most don't love what you love the most. They don't know you. Don't apologise for your dreams.”
“Sex to me is not luxury any more. It is necessity of reproduction.”
“Mwalimu Julius Nyerere was a father to his family. To Tanzania he was a defender of a dream.”
“The best prize life has to offer is not a chance to work hard and be something in the community. It is the perfume of God that resides within you.”
“Msichana wa miaka 18 miaka ya 70 ni sawa na msichana wa miaka 8 leo. Msichana wa miaka 8 leo anayajua maisha kuliko msichana wa miaka 18 miaka ya 70. Tuwape watoto wetu haki yao ya msingi ya kuwa watoto katika siku za ujana wao, kabla hawajawa watoto tena watakapokuwa wakubwa.”
“Watu hawaheshimu wewe ni nani au unatoka wapi. Wanaheshimu nguvu ya matendo yako.”
“Kufanikiwa katika maisha ni kuwa tayari muda wowote kujitoa mhanga kwa ajili ya kitu unachoweza kuwa.”
“Kitu cha kwanza kufanya kama umeamua kuficha ukweli wape watu ukweli mwingine.”
“Nafasi yako peponi itapotea iwapo utamruhusu Pluto (kiongozi wa ahera) akukaribishe bazarai (makao makuu ya ahera) kwa kuchukua maisha yako mwenyewe. Kujiua ni kujipenda zaidi kuliko unaowapenda. Anayejiua hujifikiria zaidi yeye kuliko wengine.”
“Rais wa Tume ya Dunia hakuchaguliwa kuwa kitu katika tume. Alichaguliwa kufanya kitu katika dunia.”
“Addiction isn't about using drugs. It's about what the drug does to your life.”
“People don't follow ordinary people; they follow extraordinary people.”
“Kujiua ni ubinafsi kwa sababu ya watu wanaokupenda.”
“Gari hii ni nzuri kuendesha.”
“Ukiishi Mexico City katika daraja la watu wakubwa na wewe na anasa ni marafiki wakubwa, hutapenda kuendesha gari ambayo kila mtu anaendesha mjini. Nunua gari na kuibadilisha kuwa ya kwako. Lisa aliponunua gari yake huko Ejército Nacional Mexicano, Mexico City, katika duka la Ferrari, aliipeleka Los Angeles kwa marekebisho aliyoyataka. Ferrari haikuwa ya kawaida. Mbali na kinga ya risasi ya inchi nne, Ferrari ya Lisa ilikuwa na mwendo mkali na matairi makubwa kuliko Ferrari za kawaida. Ilikuwa na rangi tatu: nyeusi, pinki na njano zilizokuwa zikibadilika kulingana na hali ya hewa; na kadhalika ilikuwa na breki ya upepo kwa nyuma, katika buti ya aluminiamu, kwa ajili ya kuikandamiza chini wakati wa mwendo mkali, ili isiyumbe sana barabarani. Lisa peke yake ndiye aliyekuwa na gari ya namna hiyo Mexico City nzima.”
“Usalama wa Taifa ni akili si ukali. Kazi yake, au wajibu wake; ni kukusanya, kuchanganua, kudurusu na kuunganisha kwa makini, taarifa nyeti za kijasusi za ndani na nje ya nchi kuilinda Tanzania na watu wake. Ukitaka kuwa na akili kuwa kawaida. Ukitaka kuwa na nguvu kuwa mkarimu. Ukitaka kuwa tajiri kuwa tajiri wa unyenyekevu.”
“Watu wanaohatarisha maisha yao kwa kudharau sheria wakati mwingine hawatakiwi kudharauliwa. Ni sawa na mtu aliyepoteza kila kitu katika maisha yake. Wana uwezo wa kufanya chochote.”
“Kolonia Santita ni kitabu cha Kiswahili. Si Kingereza wala Kihispania. Lazima tujifunze kuipenda na kuitetea lugha yetu kwa manufaa ya vizazi vijavyo.”
“Iwapo kila mtu atamheshimu mwenzake kama anavyojiheshimu mwenyewe; tunaweza kuishi mbinguni duniani ... lakini kwanza tuwe na maarifa binafsi.”
“Migogoro inatokea kwa sababu watu wameshindwa kuheshimiana. Ukijiheshimu na ukaheshimu wengine; utaacha dunia katika hali nzuri kuliko ulivyoikuta, wakati ukiingia.”
“Acha dunia katika hali nzuri kuliko ulivyoikuta.”
“Katika jiji la Dar watu hawaendi kazini. Wanakwenda vitani. Wania kilicho chako ukidhulumiwa. Utajiri humpendelea anayejaribu.”
“Vichwa vitatu vya sururu na chembe tatu za bunduki za Kalashnikov; na alama ya bahati, mafanikio, udhalimu na mwanzo mpya ya msalaba wa swastika, kama alama ya ujenzi na uhalifu wa Kolonia Santita.”
“Kila mtu hapa duniani ni jirani yako. Hakuna mtu mwingine hapa ulimwenguni isipokuwa sisi. Lazima tujifunze kuishi pamoja.”
“Mihadarati ni chanzo kikubwa cha matatizo ya wanadamu. Mshahara wake ni wazimu, uhalifu na mauti.”
“Watu wanapokuwa katika migogoro maisha yao hutakiwa kurahisishwa. Kuna ukingo mwembamba kati ya uzima na wazimu.”
“Tusipambane na madawa ya kulevya peke yake. Tupambane na elimu ya madawa ya kulevya pia.”
“Kufanya kosa huku ukijua ni kosa ni kujiombea jela mwenyewe.”
“Kinachotokea leo kitatuathiri kesho. Mbegu tunazopanda sasa ni mazao ya msimu ujao.”
“Joram Kiango ni mpelelezi maarufu nchini Tanzania. Willy Gamba ni mpelelezi maarufu katika bara la Afrika. John Murphy ni mpelelezi maarufu duniani. Ni watu watatu tofauti wanaofanya kazi zinazofanana.”
“Sema hapana kwa ndiyo nyingi kwa sababu hawaoni unachokiona. Ndoto yako waijua mwenyewe.”